HULK, ROBINHO WAIZAMISHA CHILE 2-1 HUKO TORONTO, NEYMAR AIBUKA NYOTA WA MCHEZO

  HULK, ROBINHO WAIZAMISHA CHILE  2-1 HUKO TORONTO, NEYMAR AIBUKA NYOTA WA MCHEZO

Wednesday, 20 November 2013 08:21
Print PDF
>>NEYMAR HAKUFUNGA LAKINI NYOTA WA MCHEZO!!
WAFALME wa Soka Duniani, Brazil, ambao pia ndio Wenyeji wa Kombe laNEYMAR_THE_BRAZILIAN Dunia Mwaka 2014, Alfajiri hii huko Rogers Centre, Toronto, Canada waliitandika Chile Bao 2-1 katika Mechi ya Kirafiki.
Neymar, ambae hakufunga, ndie alikuwa Nyota wa mchezo wakati Brazil ikiendeleza wimbi la kutofungwa katika Mechi 12 na Chile linaloanzia Agosti Mwaka 2000.
Robinho ndie alieifungia Brazil Bao la ushindi katika Dakika ya 79 baada ya Chile kusawazisha Bao la kwanza lililofungwa na Hulk huku Mfungaji wa Chile akiwa Eduardo Vargas.
+++++++++++++++++
MAGOLI:
Brazil 2
-Hulk Dakika ya 14
-Robinho 79
Chile 1
-Eduardo Vargas Dakika ya 71
+++++++++++++++++
Ijumaa iliyopita Chile ilikuwa Mjini London Uwanja wa Wembley ambapo waliifunga England Bao 2-0 na Brazil kuwa huko Miami, USA ambako waliichapa Honduras Bao 5-0.
VIKOSI:
BRAZIL: Júlio César, Maxwell, Maicon, Thiago Silva [Dante], David Luiz, Luiz Gustavo, Paulinho [Hernanes], Oscar [Willian], Jô [Robinho], Hulk [Ramires], Neymar [Lucas Leiva]
CHILE: C. Bravo, M. González, G. Jara, E. Mena, M. Diaz [J. Beausejour], J. Fuenzalida [J. Valdivia,=M. Fernández], G. Medel, C. Carmona, F. Gutiérrez [C. Muñoz], A. Sánchez, E. Vargas
Refa: S. Petrescu

pop up

 
Support : KARIBU TENA BONGO MASKANI
Copyright © 2011. BONGO MASKANI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA BONGO MASKANI
Proudly powered by Blogger