SIKU chache baada ya kuingia katika mgogoro na msanii mwenzake, Chuchu Hans kwa madai ya kugombea penzi la Vincent Kigosi ‘Ray’, muigizaji Blandina Chagula ‘Johari’ amesema amegundua mapenzi yanaumiza na ni sumu mbaya maishani.
“Mapenzi ni kitu kingine kabisa, sikuwahi kujua ni kwa nini baadhi ya watu hufikia hatua ya kukatisha maisha yao kisa mapenzi, hakika mapenzi ni sumu kali sana maishani usipojiongoza,” alisema Johari.