MAADHIMISH​O YA SIKU YA UKIMWI MAGEREZANI TANZANIA BARA YAFANYIKA GEREZA KUU UKONGA, JIJINI DAR ES SALAAM

1g 5db61
Mdau kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Madawa ya Kulevya na Uhalifu(UNODC), Dkt. Edwin Swai akitoa Salaam katika Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Magerezani yalifanyika leo Desemba 14, 2013 ndani ya Gereza Kuu Ukonga Dar es Salaam(wa kwanza kushoto) ni Mdau kutoka Tume ya Kuthibiti UKIMWI Tanzania(TACAIDS), Jumanne Issango na wa pili kushoto ni Mdau kutoka Mpango wa Taifa wa Kuthibiti UKIMWI(NACP), Dkt. Patrick Mwidunda.
2g a6857
Kikundi cha Wasanii wa Mziki wa Kizazi kipya cha Wafungwa wa Gereza Kuu Ukonga wakitumbuiza mbele ya Mgeni Rasmi( hayupo pichani) katika Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Magerezani yaliyofanyika leo Desemba 14, 2014 ndani ya Gereza Kuu Ukonga, Dar es Salaam. Kikundi hicho kinaongozwa na Msanii Papii Kocha( wa tatu kulia)ambaye anatumikia kifungo chake Gerezani.
3g bb928
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akikabidhi cheti Maalum kwa Mmoja wa Wafungwa Waelimishaji rika kuhusu masuala ya UKIMWI na Kifua Kikuu Magerezani leo Desemba 14, 2013 katika Maadhimisho ya UKIMWI Magerezani ambayo yamefanyika ndani ya Gereza Kuu Ukonga.
4g 07706
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitoa hotuba fupi ya Maadhimisho ya UKIMWI Magerezani leo Desemba 14, 2013 kwa Wafungwa wa Gereza Kuu Ukonga, Dar es Salaam( hawapo pichani)
5g fc7bf
Wafungwa Waandishi wa Habari wa kujitegemea wa Shirika la Habari la Utangazaji la Taifa(TBC1) hawakuwa nyuma katika kuchukua matukio muhimu wakati wa Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Magerezani yaliyofanyika Gereza Kuu Ukonga Dar es Salaam leo Desemba 14, 2013

pop up

 
Support : KARIBU TENA BONGO MASKANI
Copyright © 2011. BONGO MASKANI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA BONGO MASKANI
Proudly powered by Blogger