Vanessa Mdee aka Vee Monoey ndiye msanii pekee wa Tanzania ambaye
amepata nafasi ya kutumbuiza katika show kubwa nchini Nigeria ya ‘Rythm
Unplugged 2013’ ambayo inatarajiwa kufanyika kesho na host wa show hiyo
atakuwa msanii wa Marekani Wyclef Jean.
Wyclef baada ya kuwasili Naija
Wyclef Jean tayari amewasili nchini humo kwa ajili ya show hiyo kubwa
ambayo hufanyika mara moja kwa mwaka, na kuhusisha wasanii wakubwa wa
Naija wakiwemo P-Square, Wiz Kid, Davido, D’Banj na wengine.
Jean alitweet masaa machache kabla hajaondoka Marekani,
“I am on my way to Africa today !v “Nigeria” “Ghana” We all Love
Nelson Mandela! Then I will be in Jamaica my second home performing at
“sting”.
Hii ni mara ya pili kwa Wyclef kwenda Nigeria kuhost tamasha la muziki, baada ya ile ya MTV Africa Music Awards.