 
 MTANGAZAJI wa Kituo cha Redio cha Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amewashangaza watu baada ya kutundika mtandaoni picha zinazomuonesha akioga bafuni huku nyingine akiwa chooni akikata gogo.
Picha
 hizo zinapatikana kwenye mtandao wake na hakueleza ilikuwa wapi ila 
akasema ilikuwa ni siku alipoamua kuitumia wikiendi yake ipasavyo katika
 hoteli ambayo hakuitaja jina.
 
Baadhi ya watu waliyoziona picha hizo 
walimponda wakidai eti ni ulimbukeni lakini wapo waliomtetea kwa kusema,
 ni staili tu ya maisha aliyoamua kuishi.

“Ushamba
 tu, ndo nini sasa?  alisema mmoja wa 
wadau huku mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Dick akisema: 
“Msimuonee wivu mwenzenu, anakula bata zake na nyie hamjakatazwa.”
 
Dida
 alipoulizwa kuhusu kujianika hivyo alisema, hizo ni ishu zake binafsi 
na wapenzi wake wanapenda kuona kila anachokifanya, ndiyo maana 
anawawekea kwenye blogu yake.

 
 
 
 
 
 
