DU!.. AJALI NYINGINE HII YAUA WAWILI AKIWEMO DEREVA WAWILI...!



Hii kati ya ajali ambazo zimekuwa zikitokea kila mara Tanzania
WATU
wawili wamekufa na wengine 14 kujeruhiwa baada ya basi
waliolokuwa wakisafiria la Simiyu Express kupinduka katika eneo la
Ihumwa nje kidogo ya manispaa ya Dodoma. Basi hilo lenye namba za usajili T 717 ANL aina ya scania basi lilikuwa likiendeshwa na dereva aliyetambulika kwa jina la Mramba Issa (31). Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa Susan Kaganda, alisema kuwa basi hilo lilikuwa linatokea Bariadi kwenda Dar es salaam likiwa na abiria 60 liliacha njia na
kupinduka kutokana na mwendo kasi . Kamanda alisema kwamba ajali hiyo ilitokea leo alfajiri majira ya saa tisa usiku katika barabara ya Dodoma-Dar es salaam eneo la Elshadai . Kamanda Kaganda aliwataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni
pamoja na dereva wa basi hilo Mramba Issa mkazi wa Magomeni
Dar es salaam na Frola Erenest(21) Mwalimu wa shule ya msingi Mwamoto
kolokolo, Bariadi. Aidha kamanda akizungumzia zaidi ajali hiyo alisema kwamba basi hilo lilikuwa likiwakwepa askari wa barabarani kwa kupita njia za panya. Alifafanua kuwa kwa basi hilo kusafiri usiku huo ni kukwepa askari . Aliwataka pia wamiliki wa magari kuweka madereva wawili kwa
magari ya masafa marefu na pia wazingatie sheria za barabarani.

pop up

 
Support : KARIBU TENA BONGO MASKANI
Copyright © 2011. BONGO MASKANI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA BONGO MASKANI
Proudly powered by Blogger